Tuesday, February 21, 2012

King'amuzi halisi vidoleni mwako!


KING’AMUZI HALISI ni blog ambayo ina lengo la kuibua mijadala inayokusudia kuwaelimisha wanajamii juu ya mambo mbalimbali ambayo yanatokea katika jamii yetu.Mambo hayo yaweza kuwa mema au mabaya, yaani chanya na hasi.
                Mara nyingi, mijadala hii italenga kupongeza, kukosoa na kuhamasisha watu waliopewa dhamana ya kusimamia usitawi wa jamii kupitia taasisi mbalimbali nchini. Hii ni pamoja na taasisi za kidini, kisiasa, serikali, mashirika yasiyo ya serikali na vyama vya kiraia. Msukumo mkubwa ukiwa ni maendeleo ya  jamii.

Maono
Maono ya mwanzilishi wa blog hii ni kuwa, katika miaka  michache ijayo tupate jamii yenye  watu wenye uelewa zaidi wa mambo muhimu yanayowagusa au yanayogusa maisha yao, kiuchumi,kitamaduni, kielimu, kisiasa na kijamii kwa ujumla wake. Hawa watu wawe na uwezo wa kuyatatua matatizo yanayowakabili badala ya kulalamika bila kuchukua hatua.

Malengo
Kuwaunganisha  wana jamii  kimitazamo ili wawe na lengo moja (common objective) ambalo ni chanya kwao katika wao kujiletea ustawi wa kimaisha! Nasema  lengo chanya kwao kwa sababu moja kwamba, kuna uwezekano kuwa kitu ambacho kwako ni chanya kwa mtu mwingine chaweza kuwa hasi.
               
Namna ya kushiiriki
Ili kufikia lengo lake kubwa kama lilivyoainishwa hapo juu, KING’AMUZI HALISI kinatoa uwanja mpana wa wanajamii kujadili mambo yanayowasibu, mafanikio yao na changamoto zinazowakabili na kutoa suluhu, hili si jambo lahisi.
                Mada au mijadala itaibuliwa hapa na wanajamii watatoa maoni yao juu ya mada husika.

Washiriki
Washiri wa mijadala hi ni watanzania kwa ujumla bila kujali jinsia, umri, cheo, dini ,uwezo kifedha, nk.

Mwisho
Nawaomba washiriki wate wa mada zitakazoibuliwa katika blog hii wawe wavumilivu wasio na jazba kwani jazba kama jazba haita tatua matatizo yetu, ila kuvumiliana na kutafuta njia mbadala ni jambo ambalo laweza kutufikisha mbali.

No comments:

Post a Comment