Sunday, April 8, 2012

Watawala Wamebaka Demokrasia na Uhuru wa kuchagua


 Tarehe tano mwezi wa nne mwaka hiuu, ilikuwa ni siku ya hukumu ya kesi ambayo mwakilishi wa wananchi kwa Arusha yaani mbunge wao alikuwa ameshitakiwa nayo.

Waliomshitaki walitoa madai mengi ikiwo kuiomba mahakama kutengua ushindi wa Mbunge huyo kwa madai kuwa alipata ubunge huo pasipo halali na alitumia lugha za matusi na unyanyasaji dhidi ya wanawake wa Arusha na Tanzania.

Katika muda wote huu ambapo kesi ilikuwa ikisikilizwa zaidi ya  miezi mitatu huyo anayedaiwa kudhallilishwa hajawahi kuja mahakamani ama kulalamika au hata kuthibitisha kuwa kweli alidhalilishwa.

Pamoja na watu hao kutoweza kumleta mhusika kuthibitisha jambo hilo mahakama kuu kanda ya Arusha iliridhika na kuchukua hatua ya kumvua ubunge mbunge wa Arusha na kwamba yeye si mbunge tena!

La kushangaza zaidi hukumu hiyo tayari ilisha tolewa hata kabla ya siku ya hukumu kwani polisi walikuwa wanajua kitakachotokea na walizingira ofisi ya mbunge maasa matatu - manne kabla ya muda wa hukumu!
Sasa sisi tunajiuliza walipataje kujua kuwa hukumu itamvua Mbunge huyo madaraka?

Hiyo ni siri yao na hatutaki kujua ila tulicho kiona sisi kama wananchi wa Arusha kuwa tumibakwa kidemokrasia kwa kunyimwa haki ya kuwa na kiongozi tunayemtaka kwa sababu tu ya mafisadi wa ccm!
Watu walimchagua Lema ni zaidi 50,000 hawa wote wamekatiliwa na CCM kwa kunyimwa mbunge wao isivyo halali. japo mimi si mwanasheria lakini tumesoma machapisho mengi ambayo yanaonyesha wazi kuwa hapakuwa na kifungu cha sheria kinachotoa uhalali wa mbunge huyo kuvuliwa ubunge.

Tunachokiona hapa ni kuwa tunalazimishwa kuwa na viongozi ambao hatuwataki. Pia eleweke wazi kuwa Mbunge huyo alikuwa na mipango mingi na wanchi wake, mojawapo ni wale watoto yatima waliokuwa wanasomishwa na mfuko wa maendeleo aliouanzisha, akiwa kama mbunge.

Hawa wote wamenyimwa haki yao ya kupata Elimu na mengine mengi

Sasa najiuliza tunakwenda wapi kama taifa? Je CCM wanataka kutuaminisha kuwa haki nchi hii ipo kwa wale tu wanaotakiwa na viongozi wakuu? Je hali hii ya kupoka haki za watu ikiendelea tutarajie nini?
Je hii inatufundisha nini kama watu tunaohitaji kuendelea kuwa wamoja na wenye kuheshimiana?

Kuna maswali mengi sana katika hili ambayo watu wengi wanajiuliza, lakini mwisho wa yote itakuwaje  

Mbunge wa Ubungo John Mnyika akiwa katika hali ya butwa baada ya  hukumu ya Lema







Wananchi wa Arusha wakiwa wamikusanyika mahakamani kufuatilia hukumu ya kesi hiyo

Wananchi wa Arusha pamoja na Mbunge wa Arumeru Mashariki wakifuatilia kesi





Mkutano wa wanaarusha na Mbunge wao wakijadili uonevu wa serikali

Watu wakihuzunikia maamuzi mabaya ya mahakama za CCM 

Umati wa huu unahuzunika na kutafakari uonevu wa serikali

Kweli wananchi wa Arusha wameonewa!

Friday, February 24, 2012

Je nyumba za ibada bado ni tumaini kwa ustawi wa watu?

Nyumba za ibada  
Ndugu zangu wapendwa karibuni tena katika mjadala wa leo mjadala wa leo unasema: Je nyumba za ibada bado ni tumaini kwa ustawi wa?

Katika siku za karibuni tumeshuhudia mambo mengi sana yakitokea katika jamii yetu. Miongoni mwa mambo hayo ni unyanyasaji wa wanajamii, unaofanywa kwa makusudi na serikali yetu.
Kwa sisi wenye kuamini katika Mungu, tuliangalia huku na huko, hatukuona mtetezi isipokuwa ni kulee kwenye nyumba za ibada!

Mawazo yetu hayo yalikuwa yamejikita katika imani kuwa huko kwaenye nyumba za ibada kutakuwa ni mahali pekee ambako dhuluma, uzushi, uongo, maonezi na fitina havipewi nafasi!

Lakini tunayoyaona sasa ni kinyume kabisa. Nyumba hizo zimeungana na wazushi ambao aibu imewakauka kabisa mithiri ya mto unaopitisha maji wakati wa masika tu. na sasa ni kiangazi hakuna hata harufu ya maji!

Wakiwa na akili zao timamu, wakiwa wanajua kabisa kuwa wanachotenda, si sahihi, wanachosema si kweli na hata wanacho amini si halisi, lakini huwa wanaujasiri wa hali ya juu sana katiaka kutimiza azima yao.

Nyumba za ibada yaani viongozi wa dini na madhehebu kwa kujua ama kwa kutojua wametumbukia kwenye mtego huohuo na sasa utawasikia wakiwatetea mafisadi kwa nguvu zote na hata kwa kula kiapo cha kufa! Hili ni jambo la kusikitisha sana.

Je tumwamini nani, au ndo yale ya wanamuziki? kwamba kila unayemwamini ni kigeugeu?

Amani Bandia Tanzania


King'amuzi Halisi

Ni wakait mwingine tunapo kutana tena, kwa nia moja tu ya kujulishana, kuburudishana na kuelimishana juu ya mambo mbalimbali yanayotuhusu. Kama mjuavyo kuwa kulikuwa na maandamano makubwa huko Songea na kwa kutotumia akili polisi waliwafyatulia watu risasi za moto, hivyo kusababisha watu wawili kupoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa. Hili si jambo la kujivunia hata kido!

Kwa wenye akili timamu watakubaliana na mimi kuwa hakuna amani Tanzania!

Kila kukicha vyombo vyetu vya habari hasa vinavyomlikiwa na serikali vinatuhubiria kuwa Tanzania ni nchi yenye amani.

Je hii ndio amani tunayohubiriwa kila siku?

Tafakari!

Tuesday, February 21, 2012

King'amuzi halisi vidoleni mwako!


KING’AMUZI HALISI ni blog ambayo ina lengo la kuibua mijadala inayokusudia kuwaelimisha wanajamii juu ya mambo mbalimbali ambayo yanatokea katika jamii yetu.Mambo hayo yaweza kuwa mema au mabaya, yaani chanya na hasi.
                Mara nyingi, mijadala hii italenga kupongeza, kukosoa na kuhamasisha watu waliopewa dhamana ya kusimamia usitawi wa jamii kupitia taasisi mbalimbali nchini. Hii ni pamoja na taasisi za kidini, kisiasa, serikali, mashirika yasiyo ya serikali na vyama vya kiraia. Msukumo mkubwa ukiwa ni maendeleo ya  jamii.

Maono
Maono ya mwanzilishi wa blog hii ni kuwa, katika miaka  michache ijayo tupate jamii yenye  watu wenye uelewa zaidi wa mambo muhimu yanayowagusa au yanayogusa maisha yao, kiuchumi,kitamaduni, kielimu, kisiasa na kijamii kwa ujumla wake. Hawa watu wawe na uwezo wa kuyatatua matatizo yanayowakabili badala ya kulalamika bila kuchukua hatua.

Malengo
Kuwaunganisha  wana jamii  kimitazamo ili wawe na lengo moja (common objective) ambalo ni chanya kwao katika wao kujiletea ustawi wa kimaisha! Nasema  lengo chanya kwao kwa sababu moja kwamba, kuna uwezekano kuwa kitu ambacho kwako ni chanya kwa mtu mwingine chaweza kuwa hasi.
               
Namna ya kushiiriki
Ili kufikia lengo lake kubwa kama lilivyoainishwa hapo juu, KING’AMUZI HALISI kinatoa uwanja mpana wa wanajamii kujadili mambo yanayowasibu, mafanikio yao na changamoto zinazowakabili na kutoa suluhu, hili si jambo lahisi.
                Mada au mijadala itaibuliwa hapa na wanajamii watatoa maoni yao juu ya mada husika.

Washiriki
Washiri wa mijadala hi ni watanzania kwa ujumla bila kujali jinsia, umri, cheo, dini ,uwezo kifedha, nk.

Mwisho
Nawaomba washiriki wate wa mada zitakazoibuliwa katika blog hii wawe wavumilivu wasio na jazba kwani jazba kama jazba haita tatua matatizo yetu, ila kuvumiliana na kutafuta njia mbadala ni jambo ambalo laweza kutufikisha mbali.